Jarida la Aprili 2009

Kama mnavyojua siku ya kimataifa ya familia inasherehekewa kila mwaka siku ya tarehe 15 Mei tangu mwaka 1994. Katika sehemu ya pili ya kijarida hiki tutajaribu kujiandaa kwa ajili ya siku hiyo.
Lakini kwanza tunataka kuwapa ushuhuda wa Bi. Moshi Nyashebo aliyekuwa kwa muda mrefu katika shirika la "Single Unemployed Women" (wanawake wajane na wasio na kazi) lililopo Dar es Salaam. Tunadhani sisi sote tunahitaji kujua kwamba hatuko peke yetu katika mahangaiko dhidi ya umasikini uliozidi kiasi. Raia wengi wanajitoa katika maeneo wanayokaa, wanapofanya kazi na katika mashirika. Wanajitoa kwa njia tofauti na kusikia juu ya uzoefu wao inatupa moyo wote.






